muhtasari

Latest Article Get our latest posts by subscribing this site

RUVU SHOTING YAIBANA SIMBA LIGI KUU - YATOKA SARE 1-1 NA SIMBA...


 Mshambuliaji wa Simba, Haruna Chanongo akichuana na beki wa Ruvu shooting, stephano Mwasyika. (Picha na Habari Mseto Blog)
 Amri Kiemba akichuana beki wa Ruvu Shooting, Abuu Hashim.
 Hekaheka katika lango la Ruvu Shooting.
 Mshambuliaji wa Simba, Betram Mombeki akimiliki mpira huku akizongwa na beki wa Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Golikipa wa Ruvu Shooting, Abdul Seif akiokoa moja ya hatari langoni mwake.
 Berntram Mombeki akiruka daruga la beki wa Ruvu Shooting, Abuu Hashim. 
Henry Joseph, Abel Dhaira na Joseph Owino wakiteta jambo wakati wakitoka mapumziko. PICHA NA FRNACIS NDADE

AZAM YATOKA SARE NA WAGOSI COASTAL UNION - MECHI YATAWALIWA NA VURUGU...


 Leo golikipa wa Azam Mwadini Ally alikuwa na wakati mgumu sana, ingawa bahati haikuwa ya Wagosi.


                             Yayo Kato akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Azam FC.
 Nahodha Jerry Santo akikunjuka nje kidogo ya lango la Azam, ingawa shuti lake halikuleta madhara.
 Kocha wa Coastal Union, Hemed Moroco akiwabwatukia wachezaji wake wacheze kama alivyowafunza.



 Hili ndilo bao la kipindi cha pili walilokosa Coastal Union, ambapo shuti la Selembe lilipita mikononi mwa Mwadini Ally na kugonga mwamba.


SULUHU ya bila kufungana kati ya Coastal Union na Azam FC katika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga imezidi kuwaongezea idadi ya suluhu Wagosi wa kaya katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Mchezo huo uliokuwa na presha kubwa kwa mashabiki na wachezaji ulimuweka katika wakati mgumu mwamuzi Andrew Shamba kutoka Pwani, kutokana na kushutumiwa kuwapendelea Azam FC.

Kipindi cha kwanza timu zote zilicheza kwa nguvu zikihakikisha zinapata mabao ya mapema na kujihakikishia ushindi lakini hakuna hata timu moja iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake.

Kipindi cha pili kilianza kwa Azam FC kushambulia kwa kasi huku wakimiliki mpira hali iliyowachanganya wachezaji wa Coastal Union wakaanza kupoteana na kucheza bila kufuata mfumo. Hali hiyo ilizidi kuwachanganya Wagosi wa Kaya hasa baada ya mwamuzi kuanza kutoa maamuzi ya utata, kwani katika dakika ya sabini alitoa kona kwa Azam wakati ilikuwa ni goal kick.

Mashabiki wakaanza kuhamaki na kutaka kuvuruga mchezo baada ya mwamuzi kuzidisha kutoa maamuzi ya utata kama faulo zisizoeleweka na kona za utata. Hali hiyo ilimtisha mwamuzi na kusimamisha mchezo mara kwa mara ili kuwataka wasimamizi wa mchezo huo kuwatuliza mashabiki.

Tukio lililotokea kipindi cha kwanza ambapo mwamuzi wa pembeni alipigwa na kitu kisichojulikana kutoka jukwaa la 'Rasha' lilitaka kujirudia kipindi cha pili baada ya chupa na mawe kutupwa uwanjani baada ya mwamuzi kutoa faulo nje kidogo ya 18 upande wa Coastal Union.

Dakika ya 65 mwalimu Hemed Moroco alifanya mabadiliko na kumtoa Pius Kisambale akaingia Suleiman Kassim 'Selembe'. Mabadiliko hayo yaliongeza uhai kwa Wagosi hasa kutokana na aina ya uchezaji wa Selembe kutumia mipira ya kasi.

Azam FC walianza kuelemewa kutokana na Mganda, Yayo Kato kutumia vema mwili wake mfupi na wenye nguvu kuwashambulia mabeki wa Azam, hali hiyo iliwafanya Azam kubadilika na kucheza mpira wa hovyo uliowapa nafasi Coastal Union kupiga mipira mirefu ambapo ilipofika dakika ya 75 kipindi cha pili katika jukwaa la African Sports, Wagosi walikosa bao la wazi baada ya Selembe kupiga krosi iliyopenya ngome ya Azam akiwemo mlinda mlango Mwadini Ally na kugonga mwamba.

Kutokana na piga nikupige ya lala salama kufika dakika ya 74 mwamuzi alimnyooshea mlinzi wa kulia wa Coastal Union, kinda Hamadi Juma 'Basmat', kadi nyekundu baada ya kubadilishiana maneno na mchezaji wa Azam, Kipre Tchetche.

Tukio hilo lilianzia kwa Kipre kumpiga Hamadi kiwiko cha shingo hali iliyomfanya kinda huyo kumfuata kwa jazaba huku akimuuliza kwanini amemfanyia hivyo. Mwamuzi baada ya kuona Hamadi amemuelekezea kichwa Kipre akadhani kinda huyo anapigana ndipo akatoa kadi ya moja kwa moja.

Baada ya kadi hiyo hali ya uwanja ilichafuka ambapo mashabiki walikuwa wakipiga kelele huku wachezaji wakitaka kupigana, ndipo mchezaji mwingine wa Coastal Union beki wa kushoto Othman Tamim akapewa kadi ya njano papo hapo.

Baadaye mchezo ulirudi katika hali yake lakini ngome ya Coastal Union ilikuwa imepwaya hali iliyomfanya Juma Said 'Nyoso' kuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha ngome yao inakuwa imara.

Ilipofika dakika ya 84 mwlimu Moroco alifanya mabadiliko kwa kumtoa Uhuru Suleiman na kumuingiza Yusuf Chuma. Ambapo kinda huyo alionyesha uwezo mkubwa na kurudisha uhai wa safu ya ulinzi.

Mpaka mwamuzi wa leo anapuliza kipyenga cha mwisho matokeo yaliendelea kusomeka hivyo hivyohivyo 0-0, na kuendelea kuibakisha Coastal Union katika nafasi ya nne ikiwa na point 11 nyuma ya Azam iliyo nafasi ya tatu yenye point 11 lakini ikiwa na mabao mengi ya kufunga.

Baada ya mechi ya leo Coastal Union itashuka dimbani wiki ijayo katika uwanja wa Chamazi dhidi ya Ashanti United wanaoshika mkia katika ligi
.

MTUHUMIWA AJINYEA MAHAKAMANI WAKATI AKISOMEWA KIFUNGO CHA MIEZI 6 JELA JIJINI DAR...



 
 
Mtu mmoja amehukumiwa kifungu cha miezi sita jela katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Sokoine Drive kwa kosa la kujisaidia haja kubwa ndani ya Mahakama wakati akisomewa mashitaka. 

Adhabu hiyo ilitolewa papo hapo baada ya mshitakiwa Hassan Omary (25) kufanya kitendo hicho aliposomewa mashitaka mengine tofauti.
 
Hakimu William Mutaki ndiye aliyetoa hukumu hiyo. Wakati akisomewa mashitaka sanjari na washitakiwa wengine watatu ya kubughudhi abiria maeneo ya Kariakoo, Omary inadaiwa alitokwa haja kubwa.
 
Mwandishi alishuhudia mshitakiwa huyo akisafisha eneo la mahakamani alikochafua kabla ya kupelekwa jela. Wengine anaoshitakiwa nao katika kesi hiyo ni Mohamedi Mussa (20),Hassani Ramadhani (18),Shukuru Adison (26) na Ally Omary (28).

Mwendesha mashitaka wa serikali John kijumbe alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi William Mutaki kuwa washitakiwa walitenda kosa la kuwanyanyasa na kuwabugudhi abiria ,Septemba 18 ,mwaka huu Kariakoo, jijini Dar es Salaam. Washitakiwa wengine walirudishwa rumande hadi Oktoba 2,mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
 
Katika kesi nyingine, mshitakiwa Jacob Sasita (28) amehukumiwa kifungo cha mwezi mmoja baada ya kukiri kuwanyanyasa abiria .
 
Sasita alikuwa miongoni mwa washitakiwa saba waliofikishwa mahakamani kwa kosa hilo. Washitakiwa wengine ni Ramadhani Juma (38),Abeid Ismail (25),Abuu Rajabu(25),Salimu Kijimbo (39),Ally Hassani (28),Josephb Chambo (29)na Fabiani Thomas (28) ambao walikana kutenda kosa baada ya kusomewa mashitaka.
 
Mbele ya Hakimu Mkazi Timoth Lyon, Mwendesha Mashitaka wa Serikari, Richard Magudi alidai watu hao walitenda kosa la kuwanyanyasa abiria katika kituo kikuu cha mabasai cha Ubungo ,kabla ya kukamatwa na askari polisi. Walirudishwa rumande hadi Oktoba 2 mwaka huu kesi itakapotajwa tena.

MATOKEO KAMILI YA MICHEZO YOTE YA LIGI KUU: SIMBA YAZIDI KUTAKATA - AMIS TAMBWE APIGA MABAO MANNE MNYAMA AKIUA 6-0. YANGA YAZIDI KUKAZIWA MBEYA, AZAM FC MAMBO BADO MAGUMU...


YANGA 1 - 1 Prisons,

SIMBA 6 - 0 Mgambo

Kagera 2 - 1 JKT Oljoro

Azam 1 - 1 Ashanti

Coastal 1 - 1 Rhino

Mtibwa 0 - 0 MBEYA City

Ruvu Shooting 1 vs 0 JKT Ruvu

SIMBA VS MGAMBO: SIMBA IKO KAMILI, MGAMBO YACHIMBA MKWARA...


BAADA ya kuisambaratisha Mtibwa Sugar katika Ligi Kuu ya Bara wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba imesema kikosi chake kipo kamili kambini kuikabiri JKT Mgambo hapo kesho.

Simba inatarajiwa kushuka kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kesho kuvaana na Mgambo ikiwa na kumbukumbu ya kuifunga Mtibwa Sugar mabao 2-0 katika uwanja huo.

Matokeo hayo yaliifanya Simba ifikishe pointi saba baada ya kucheza mechi tatu na kutoka sare moja kisha kushinda mechi mbili.

Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga ameuambia mtandao huu kwamba kikosi cha timu yake kipo tayari kwa mechi dhidi ya Mgambo na kocha Abdallah Kibadeni hana wasiwasi na kikosi chake.

“Timu iko vizuri kambini Bamba Beach kujiaindaa na mchezo dhidi ya Mgambo, kocha (Kibadeni) amesema kikosi kipo tayari kwa mchezo na hakuna kitu kitakachozuia ushindi hivyo nawaomba wapenzi wa Simba wajitokeze kwa wingi uwanjani kushuhudia timu yao ikipata pointi tatu nyingine.

“Unajua mechi dhidi ya Mtibwa ilikuwa ngumu sana kwetu maana mwaka jana kama unakumbuka walitufunga na sisi msimu huu tumeweza kulipa kisasi na sasa atakayekaa mbele yetu tutahakikisha tunamfunga ili kuweza kujiweka katika mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa,” alisema Kamwaga.

Kamwaga amesema hadi sasa kikosi chake hakina majeruhi hata mmoja na wachezaji wote wapo tayari kwa mchezo. “Hatuna majeruhi hta mmoja na hata wale wenye majeraha madogo hawawezi kushindwa kujumuhishwa kikosini,” alisema Kamwaga.

Tangu mechi za msimu huu zianze Simba imekuwa ikiwategemea zaidi wachezaji wake wapya kama Issa Rashidi ‘Baba Ubaya’, Gilbert Kaze, Joseph Owino katika nafasi ya ulinzi huku katika kiungo ikiwategemea Twaha Ibrahim na Henry Joseph na kwa upande wa washambuliaji wapo Amisi Tamwe na Betram Mwombeki.

Msimu uliopita Simba ilishika nafasi ya tatu na kuziacha Yanga na Azam zikitwaa nafasi za juu ambapo Yanga ndiyo iliyotwaa ubingwa, hivyo Simba msimu huu imekosa nafasi ya kuiwakilisha nchi katika michuano ya kimataifa inayosimamiwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf).

Mgambo inayocheza na Simba hapo kesho, yenyewe ina pointi tatu tu huku ikiwa nafasi ya tisa baada ya kucheza mechi tatu na kushinda moja huku ikifungwa mechi mbili.

MGAMBO YAIVIMBIA SIMBA

Licha ya timu yake kufungwa mechi mbili za Ligi Kuu ya Bara na kushinda mechi moja tu na kujikuta ikishika nafasi ya tisa ikiwa na pointi tatu tu, Kocha wa Mgambo, Mohamed Kampira amesema kamwe Simba isitarajie mteremko katika mchezo wa kesho.

Kampira ameuambia mtandao huu kwamba, timu yake ipo jijini Dar es Salaam tangu wikiendi iliyopita na wameshafanya mazoezi ya kutosha kuweza kuibuka na ushindi hapo kesho.

“Sitishwi na matokeo yaliyotokea huko nyuma wala ukubwa wa timu ninayopambana nayo (Simba), mimi kazi yangu nimeshaifanya na wachezaji wangu sasa wapo tayari kwa mchezo ninachosubiri ni muda ufike ili tucheze na Simba,” alisema Kampira.

Kampira alisema kikosi chake hakina majeruhi wa kutisha kwani wachezaji wote wanaweza kupambana katika mechi ya kesho. “Sina majeruhi wa kutisha kwani wapo wachache wanaosumbuliwa na majeraha madogo madogo ambayo yanaweza kuwafanya wacheze,” alisema Kampira.

Popular Post

 
Support : OBAMA | OBAMA | OBAMA
Copyright © 2013. DiraYaLeo - All Rights Reserved
Template Created by Barakaeli Aremu Published by Dira Ya Leo
Proudly powered by Blogger