muhtasari

Home » » POLISI APANDISHWA KIZIMBANI BAADA YA KUNASWA NA MENO YA TEMBO YENYE THAMANI YA TSH. MILIONI 121.5...!!

POLISI APANDISHWA KIZIMBANI BAADA YA KUNASWA NA MENO YA TEMBO YENYE THAMANI YA TSH. MILIONI 121.5...!!

Askari wa Jeshi la Polisi, Ramadhan Selemani (27), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shitaka la kukutwa na meno ya tembo yenye thamani ya Sh. Milioni 121.5.

 Mbali na Selemani, mshitakiwa mwingine katika kesi hiyo ni raia ambaye anatambulika kwa jina la Hamis Mwanya (22), ambao walifikishwa jana mahakamani hapo mbele ya Hakimu Nyigulila Mwanseba.

Wakili wa Serikali, Mwanaisha Komba, alidai mbele ya Hakimu Mwanseba kuwa Julai 19, mwaka huu katika eneo la Tazara wiliyani Temeke, jijini Dar es Salaam, washitakiwa hao walikutwa na nyara za serikali ambazo ni meno ya tembo manne pamoja na vipande 12 vya meno hayo vilivyo na thamani ya Sh. milioni 121.5, ambayo ni mali ya Serikali.

Hata hivyo, washitakiwa hao hawakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi isipokuwa Mahakama Kuu na pia upelelezi wa shauri hilo haujakamilika.

Hakimu Mwanseba aliahirisha shauri hilo hadi Agosti 7, mwaka huu, na washitakiwa walirudihswa rumande.

Popular Post

 
Support : OBAMA | OBAMA | OBAMA
Copyright © 2013. DiraYaLeo - All Rights Reserved
Template Created by Barakaeli Aremu Published by Dira Ya Leo
Proudly powered by Blogger