muhtasari

Home » » WALIOFELI KIDATO CHA PILI KURUDIA UPYA KIDATO HICHO..!!

WALIOFELI KIDATO CHA PILI KURUDIA UPYA KIDATO HICHO..!!

  Serikali imeendelea kuwasisitizia wazazi na wanafunzi shuleni kuwa wanafunzi wote 136,000 waliofeli kidato cha pili mwaka jana na kutakiwa kurudia darasa hilo wanapaswa kufanya hivyo bila kushurutishwa.Imesema wasijidanganye kuwa watafanya mitihani ya kumaliza kidato cha nne mwakani kwani namba zao hazipo.

Pia wanafunzi hao wasije wakarubuniwa na baadhi ya walimu wakuu wa sekondari nchini kuwa licha ya kufeli kwao wanaweza kuendelea na kidato cha tatu mwaka huu kwani hawataweza kufanya mitihani ya Taifa ya kidato cha nne mwakani kama wanavyodhani kutokana na namba na majina yao tayari zimeondolewa katika orodha hiyo ya mwakani.

Tahadhari hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo wakati akifungua mafunzo ya Waratibu Elimu kata Kitaifa yanayoendeshwa na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) huko wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

Mulugo alisema ana taarifa ya kuwapo kwa baadhi ya wanafunzi kati ya hao 136,000 ambao wameshawishiwa na wakuu wa shule pamoja na wazazi wao kadhaa kuendelea na kidato cha tatu kwa matumaini ya kuwa watafanya mitihani ya kumaliza kidato cha nne mwaka ujao imani ambayo Waziri alisema itakuja kuwaliza baadaye maana kundi hilo halina nafasi ya kuhitimu mwakani.

Kutokana na hali hiyo Naibu Waziri Mulugo aliwaagiza waratibu elimu kata nchini wafuatilie mara moja wanafunzi wote wa kidao cha pili waliofeli kama wamekariri darasa hilo.

Alisema wanafunzi waliokaidi na kuendelea kidato cha tatu mwaka huu watoe taarifa mapema ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao na walimu waliohusika na udanganyifu huo.

Waratibu elimu kata mtakapo toka hapa kwenye mafunzo, nawaagiza sasa mkaanze na hili la kuwakufuatilia wanafunzi waliofeli kidato cha pili mwaka jana. kama wote wamerudia darasa au wanaendelea na kidato cha tatu,”alisema Mulugo.

Awali Ofisa Taaluma wa Mkoa wa Dar es Salaam Benadeta Thomas alisema mafunzo hayo yanaendeshwa katika mikoa 11 nchini na ni utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari ngazi za kat.

Popular Post

 
Support : OBAMA | OBAMA | OBAMA
Copyright © 2013. DiraYaLeo - All Rights Reserved
Template Created by Barakaeli Aremu Published by Dira Ya Leo
Proudly powered by Blogger