Home »
» Kwanini JK (Kanali nusu mstaafu) hana ushawishi kwa Kagame (Jenerali Mstaafu)?
Posted by Unknown
Posted on Saturday, August 03, 2013
Vita vya maneno kati ya JK na
Kagame vinaasharia jinsi ambavyo Kagame haoni kama JK ana ushawishi au
hata ufahamu wa historia ya Rwanda na hivyo kumkejeli jinsi ambavyo
anaona inafaa. Kagame ameahidi kumvutia pumzi JK na akipata mwanya
atamzabua kofi kutokana na JK kumshauri Kagame kukaa mezani na waasi wa
Rwanda.
Kagame ni vigumu kuthamini ushauri wa JK kwa sababu zifuatazo:-
1) JK haifahamu vizuri historia ya Rwanda ambayo imejengwa kwa damu.
Watutsi ambao ni wachache wametumia damu kuwatawala wahutu ambao ni
wengi na jinsi ya kuwawezesha wengi (Wahutu) bila kuathiri haki za
wachache (Watutsi) ndani ya Rwanda imeshindikana hadi leo. Mfupa uliomshinda Mzee fisi je JK atauweza kwa utendaji huu tunaoufahamu hapa nchini?
a) JK kushauri mahasimu hao wakae meza moja bila ya kujua ajenda na
mikakati ya kufanikisha vikao tajwa kwa Kagame anaona ni upuuzi ambao
mjenga hoja -JK- lazima azabuliwe kofi ili aache kujiingiza kwenye mambo
yasiyomhusu.
b) JK katika masuala ya Muungano na kero zake amekuwa akiendelea
kutegemea kamati ya viongozi wa kitaifa watokanao na chama chake cha CCM
tu bila ya kutafuta wapinzani katika kushauriana nao. Hivyo aidha ni
unafiki au usahaulifu tu kumshauri Kagame afanya yale ambayo yeye
mwenyewe JK hana mpango wa kuyafanya. Charity always begin at home.................
c) JK katika uundaji wa kamati ya marekebisho ya katiba katumia ubabe wa
uwingi wa wabunge wa CCM Bungeni katika kupitisha sheria ambayo imempa
yeye madaraka ya kurekebisha Katiba atakavyoona inafaa na ushirikishwaji
wa wananchi ni changa la macho tu. Sasa yawaje amshauri Kagame kujenga
mazingira ya ushirikishwaji wa mahasimu wake jambo ambalo yeye mwenyewe
JK hayuko tayari kulifanya. Tena hapa nchini ingelikuwa ni rahisi zaidi
kwa JK kwani hakuna umwagaji wa damu katika wananchi kudai haki zao za
kimsingi zaidi ya ukatili wa polisi ambao anayo mamlaka ya kuwakemea na
wala hana mpango wa kufanya hivyo..
d) Katika kero za Muungano, JK aliwahi kudiriki kusema kamati ya
kushughulikia kero tajwa na kuundwa na chama kimoja tu cha CCM wawe
wanakutana angalau mara nne kwa mwaka hata kama hawana la kujadili
ikimaanisha tu yeye JK anacheza mchezo wa siasa wa kuonyesha raia kazi
inafanyika hata kama hakuna linaloendelea! Mbali ya hilo, JK hana
mkakati wa kuzimaliza kero za Muungano nje ya CCM na ndiyo maana hawezi
kufiria muundo mbadala wa kutafuta ufumbuzi wa kero za muungano nje ya
chama chake sasa iwaje amtarajie Kagame atafute ufumbuzi wa kero za
Rwanda nje ya chama chake cha RPF?
e) JK hana taswira ya
kuutetea na kulinda utawala bora na ndiyo maana katika kipindi chake
mauaji yanayofanywa na polisi hadi leo yanazidi yale yaliyofanywa na
maraisi wote waliomtangulia.
Pia, katika historia ya nchi yetu kamwe Waziri Mkuu hajawahi kutamka
hadharani kuwa ni sahihi kwa polisi kupiga raia wanaodai haki zao. Hadi
wa leo, JK yuko kimya na wala hajamchukulia Pinda hatua yoyote ile
ikiashiria anaafiki udhulumaji wa haki za kimsingi kabisa za binadamu!
Hivi kwa kisa kipi Kagame amsikilize JK ambaye hana rekodi yoyote ile ya
kuheshimu utawala bora?
2) Chaguzi ya Uraisi
2010 kuna utata mkubwa kati yake na Dr. Slaa ni nani alishinda Uraisi
kutokana na Tume ya uchaguzi kufanya kazi kwa minajili ya kulinda
masilahi ya CCM huku ikishirikiana na Idara ya Usalama pamoja na
serikali za mitaa.
Kagame pamoja na faulo zake kibao, hakuna anayemtilia mashaka ya uhalali
wa chaguzi zote zilizomsimika madarakani. Kwenye mazingira ya namna
hii, ni JK au Kagame ambaye anastahili kuwekwa darasani na mwenzie juu
ya utawala bora?
3) Viongozi wengi wa TZ hususani CCM hukimbilia kutatua matatizo ya nje
ya chi yetu na kutumia sarakasi hizo kufunika matatizo ya hapa nchini
lakini wasichojua ni kuwa ili waheshimike ndani na nje ya mipaka ya nchi
hii ni pale watakapoanza kutatua kwa dhati matatizo ya hapa ndani na
kuyapatia ufumbuzi wa kudumu bila ya kujali masilahi ya muda mfupi ya
vyama vyao.
4) Kwa karata hizi ni dhahiri Kagame yuko sahihi kabisa kumbeza JK kwa kumtishia na kunuia kumzabua kofi kwa kile ambacho ni "kiherehere"
cha JK kujiingiza katika tanuru la moto la wengine wakati hapa nyumbani
moshi unafukuta kila mahali na JK haonyeshi hata dalili kujua majibu ya
kero zetu yako katika nyanja ipi.
chanzo: jamii forums