muhtasari

Home » » DAWA ZA KICHOCHO SHULENI ZAMWATHIRI MWANAFUNZI PEMBA…

DAWA ZA KICHOCHO SHULENI ZAMWATHIRI MWANAFUNZI PEMBA…

Kufanya shughuli kama vile usafi na kufua kwenye vyanzo vya maji kunaweza sababisha mlipuko wa ugonjwa wa kichocho.
Mwanafunzi wa darasa la tano wa shule ya msingi Pandani kisiwani Pemba, Asha Hamad Khalfan (13), ameathirika macho na kichwa baada ya kudaiwa kupewa dawa aina tatu tofauti na mwalimu wake ikiwemo ya kichocho, matende na malaria bila kanuni za matibabu kuzingatiwa.
Akizungumza na Mwananchi Jumapili, baba wa mwanafunzi huyo Hamad Khalfan, alisema :
“Alianza kupata homa kali mara baada ya kunyweshwa dawa hizo zikiwemo dawa za mabusha na matende, kichocho na malaria. Kwa mujibu wa maelezo yake, alipewa na mwalimu wake shuleni.”
Hamad alisema kinachomshangaza ni mtoto wake kupewa dawa hizo na mwalimu wake badala ya mtaalamu wa afya na tiba.
Alisema kwamba mtoto wake amevimba macho na sehemu ya kichwa kulegea na kuwa mithili ya kichwa cha mtoto mchanga na alilazwa katika Hospitali ya Wete kwa siku 12 kabla ya kuhamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya.
Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja mjini Unguja, Hassan Makame alithibitisha kumpokelewa mgonjwa huyo, alikanusha kukupewa dawa aina tatu kwa wakati mmoja .
Waziri wa Afya wa SMZ Juma Duni Haji alisema kwa mujibu wa kanuni za afya, dawa za aina yoyote ikiwemo ya chanjo hutakiwa kutolewa na Ofisa wa Afya mhusika.

Popular Post

 
Support : OBAMA | OBAMA | OBAMA
Copyright © 2013. DiraYaLeo - All Rights Reserved
Template Created by Barakaeli Aremu Published by Dira Ya Leo
Proudly powered by Blogger